TSK

TSK · Marko 13:32

Treasury of Scripture Knowledge references in Swahili NT.

Back to passage

"Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye.

Kisha Yesu akasema, "Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.

Hapo watamwona Mwana wa Mtu akija katika mawingu kwa nguvu nyingi na utukufu.

Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.

Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,