Saa ya sasa
Saa ya Tisa - None
Tunakumbuka kifo cha wokovu cha Kristo msalabani na toba ya yule mwivi aliyeomba kukumbukwa katika Ufalme Wake.
Utangulizi wa Kila Saa
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu
Mungu mmoja. Amina.
Bwana utuhurumie. Bwana utuhurumie. Bwana tubariki. Amina.
Utukufu kwa Baba na kwa Mwana na kwa Roho Mtakatifu, sasa na sikuzote na hata enzi za enzi. Amina.
BABA YETU
Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
Sala ya Shukrani
Na tumshukuru Mtenda mema mwenye huruma, Mungu, Baba wa Bwana wetu na Mungu wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kwa kuwa Ametufunika, Ametusaidia, Ametuhifadhi, Ametukaribisha kwake, Ametuhurumia, Ametutia nguvu, na Ametuletea hadi saa hii. Tena na tumwombe pia Atuhifadhi katika siku hii takatifu na siku zote za maisha yetu kwa amani kamili. Mwenyezi, Bwana Mungu wetu.
Ee Bwana Mungu Mwenyezi, Baba wa Bwana wetu na Mungu wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo, tunakushukuru kwa kila hali, na kwa ajili ya kila hali, na katika kila hali; kwa kuwa Umetufunika, Umetusaidia, Umetuhifadhi, Umetukaribisha kwako, Umetuhurumia, Umetutia nguvu, na Umetuletea hadi saa hii.
Kwa ajili ya haya tunaomba na kusihi kwa wema Wako, Ee Mpenda wanadamu, utujalie tumalize siku hii takatifu na siku zote za maisha yetu kwa amani kamili pamoja na kumcha Wewe. Kila wivu, na kila jaribu, na kila tendo la Shetani, na shauri la watu waovu, na kusimama kwa adui waliofichika na walio dhahiri, uyatoe mbali nasi na mbali na watu Wako wote, na mbali na mahali pako hapa patakatifu. Na yaliyo mema na yafaa, utujalie. Kwa kuwa Wewe Ndiwe Uliye tupa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na kila nguvu ya adui. Wala usitutie majaribuni, bali utuokoe na yule mwovu.
Kwa neema na rehema na upendo kwa wanadamu ulioko kwa Mwanao wa pekee, Bwana wetu na Mungu wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Yeye ambaye kwa kupitia kwake, utukufu, heshima, enzi na ibada vinakufaa pamoja Naye, pamoja na Roho Mtakatifu, Mwenye kuhuisha, anaye Kulingana Nawe, sasa na sikuzote na hata enzi za enzi. Amina.
ZABURI 50
Ee Mungu, unirehemu kwa wingi wa fadhili zako، na kwa wingi wa rehema zako ufute maovu yangu.
Nioshe kabisa na kunitakasa dhambi yangu، kwa maana mimi najua maovu yangu، na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
Nimekukosea wewe peke yako، na kufanya yaliyo maovu mbele zako، ili uonekane mwenye haki katika maneno yako، na kuwa safi katika hukumu yako.
Tazama، mimi nalizaliwa katika uovu، na mamangu alinitunga mimba katika dhambi.
Tazama، wapenda kweli ya moyoni؛ unifundishe siri za hekima yako.
Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi؛ unioshe nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
Unisikilizishe furaha na shangwe، ili mifupa uliyoivunja ifurahi.
Ufiche uso wako usitazame dhambi zangu، na kufuta maovu yangu yote.
Ee Mungu، uniumbie moyo safi، na upya roho iliyo thabiti ndani yangu.
Usinitupe mbali na uso wako، wala usiniondolee Roho wako Mtakatifu.
Unirudishie furaha ya wokovu wako، unitegemeze kwa roho ya wepesi؛ ndipo nitawafundisha wakosaji njia zako، na wenye kosa watakurejea.
Uniokoe na hatia ya damu، Ee Mungu، Mungu wa wokovu wangu؛ ndipo ulimi wangu utaimba haki yako.
Ee Bwana، yafumbue midomo yangu؛ na kinywa changu kitasimulia sifa zako.
Maana hukufurahishwa na dhabihu؛ la sivyo ningekupa؛ wala hupendezwi na sadaka za kuteketezwa.
Sadaka za Mungu ni roho iliyovunjika؛ moyo uliovunjika na kunyenyekea، Ee Mungu، hutaudhaarau.
Uifanyie mema Sayuni kwa radhi zako، ujenge kuta za Yerusalemu.
Hapo ndipo utakaporidhika na dhabihu za haki، sadaka za kuteketezwa na dhabihu kamili؛ ndipo ng’ombe watakapotozwa juu ya madhabahu zako.
Haleluya.
Mwanzo wa Sala
Tazama ya Saa ya Tisa ya mchana uliobarikiwa, naiwasilisha kwa Kristo Mfalme wangu na Mungu wangu, nami namwomba anisamehe dhambi zangu.
ZABURI 95
Mwimbieni Bwana wimbo mpya؛ nchi yote imwimbie Bwana؛ mwimbieni Bwana na kulihimidi Jina lake.
Hubirini kutoka siku hata siku habari za wokovu wake.
Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa، maajabu yake kati ya watu wote.
Kwa maana Bwana ni mkuu، na astahili kusifiwa sana؛ ni wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
Maana miungu yote ya watu ni sanamu؛ lakini Bwana ndiye alizifanya mbingu.
Heshima na adhama ziko mbele zake؛ nguvu na uzuri zimo patakatifu pake.
Mpeni Bwana، enyi jamaa za watu، mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Mpeni Bwana utukufu wa Jina lake؛ leteni sadaka، mkaingie katika nyua zake.
Msujudieni Bwana katika uzuri wa utakatifu; nchi yote na itetemeke mbele zake.
Semeni miongoni mwa mataifa، Bwana ametawala juu ya mti؛ naam، ulimwengu umethibitishwa، hauwezi kutikisika؛ atawahukumu watu kwa adili.
Mbingu na zifurahi، nchi na icheze؛ bahari na ivume، na vyote vilivyomo;
Mbuga na zifurahi، na vyote vilivyomo ndani yake؛ ndipo miti yote ya mwituni itaimba kwa furaha mbele za Bwana؛ kwa maana anakuja، maana anakuja kuihukumu dunia; ataihukumu dunia kwa haki، na mataifa kwa uaminifu.
Haleluya.
ZABURI 96
Bwana ametawala؛ nchi na ishange؛ visiwa vingi na vikaribishe.
Mawingu na giza ziko kumzunguka؛ haki na hukumu ni msingi wa kiti chake cha enzi.
Moto hutangulia mbele zake، na kuwateketeza adui zake pande zote.
Umeme wake uliangaza ulimwengu؛ nchi ikaona، ikatetemeka.
Milima iliyeyuka kama nta mbele za Bwana؛ mbele za Bwana wa dunia yote.
Mbingu zikatangaza haki yake؛ na watu wote wakaona utukufu wake.
Aibu iwashukie wote waabuduo sanamu، wanaojisifia kwa vitu visivyo kitu؛ msujudieni Yeye، enyi miungu yote.
Sayuni ilisikia، ikafurahi؛ na binti za Yuda wakashangilia، kwa sababu ya hukumu zako، Ee Bwana.
Maana wewe، Ee Bwana، U mkuu juu ya dunia yote؛ Umeinuliwa sana juu ya miungu yote.
Ninyi mnaompenda Bwana، chukieni uovu؛ Yeye huwahifadhi roho za watauwa wake؛ huwaokoa na mkono wa waovu.
Nuru imemea kwa mwenye haki، na furaha kwa wanyofu wa moyo.
Furahini katika Bwana، enyi wenye haki؛ lisifuni Jina lake takatifu.
Haleluya.
ZABURI 97
Mwimbieni Bwana wimbo mpya؛ kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu؛ mkono wake wa kuume، na mkono wake mtakatifu، umemletea wokovu.
Bwana ameujulisha wokovu wake؛ ametangaza haki yake mbele ya mataifa.
Amezikumbuka rehema zake kwa Yakobo، na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli; miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Mungu wetu.
Pigeni vigelegele kwa Bwana، nchi yote؛ imbeni na kuimba kwa furaha na kuimba zaburi.
Imbeni Bwana kwa kinubi؛ kwa kinubi na sauti ya uimbaji.
Kwa tarumbeta na sauti ya baragumu، pigeni vigelegele mbele za Mfalme، Bwana.
Bahari na ivume na vyote viijazavyo؛ dunia na wakaao ndani yake.
Mito itapige makofi؛ milima pia itaimba pamoja kwa furaha mbele za Bwana؛ kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
Ataihukumu dunia kwa haki، na mataifa kwa adili.
Haleluya.
ZABURI 98
Bwana ametamalaki; mataifa na yatetemeke.
Akikaa juu ya makerubi; nchi naitetemeke.
Bwana ni mkuu katika Sayuni, ametukuka juu ya mataifa yote.
Na walipe jina lake kuu shukrani, kwa kuwa ni la kuogofya na takatifu; na fahari ya mfalme ni kupenda haki; wewe umeweka usawa; wewe umetenda hukumu na haki katika Yakobo.
Mmtukuze Bwana Mungu wetu, msujudie paala pa miguu yake; kwa kuwa yeye ni mtakatifu.
Musa na Haruni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, na Samweli miongoni mwa waliolilia jina lake; walimwomba Bwana, naye akawajibu.
Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao; kwa kuwa waliishika shuhuda zake, na amri alizowapa.
Ee Bwana Mungu wetu, uliwajibu; ukawa Mungu wa kuwasamehe, na mwenye kulipiza kisasi kwa matendo yao.
Mmtukuze Bwana Mungu wetu, msujudie mlimani pake mtakatifu; kwa kuwa Bwana Mungu wetu ni mtakatifu. Haleluya.
ZABURI 99
Mpigieni Bwana vigelegele, nchi yote. Mtumikieni Bwana kwa furaha, njoni mbele zake kwa kelele za shangwe. Jueni ya kuwa Bwana ndiye Mungu wetu; ndiye aliyetuumba, wala si sisi wenyewe; na sisi tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru, na nyuani mwake kwa nyimbo za sifa; mshukuruni, lihimidini jina lake. Kwa kuwa Bwana ni mwema; rehema zake ni za milele, na uaminifu wake vizazi hata vizazi. Haleluya.
ZABURI 100
Rehema na hukumu nitakuimbia, Ee Bwana; nitakuimbia sifa. Nitatumia akili katika njia iliyo bila lawama; utakuja lini kwangu? Nitakwenda kwa unyofu wa moyo wangu nyumbani kwangu. Sitaweka mbele ya macho yangu neno la uovu; wafanyao uovu nawachukia; moyo wa ukaidi hautanishikamana; mtu mwovu nikiondoka nami simjui; Amsemao mwenzake kwa siri nitamwangamiza; mtu mwenye kiburi cha macho na majivuno ya moyo sitastahimiana.
Macho yangu yatakuwa juu ya waaminifu wa nchi ili wakae pamoja nami; aendaye katika njia iliyo kamili, huyo atanitumikia. Mwenye kiburi hatakaa ndani ya nyumba yangu; asemaye uovu hatasimama mbele ya macho yangu. Kila asubuhi nitawaharibu wote waovu wa nchi, niwamalize katika mji wa Bwana wote watendao uovu. Haleluya.
ZABURI 109
Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti mkono wangu wa kuume, hata niwafanye adui zako wawe kiti cha miguu yako. Bwana atakutumea fimbo ya uweza toka Sayuni; tawala kati ya adui zako. Watu wako watakuwa wanyofu siku ya nguvu zako, kwa uzuri wa watakatifu. Tangu tumbo, kabla ya nyota ya asubuhi nimekuzaa.
Bwana ameapa, wala hatatubu: Wewe ndiwe kuhani hata milele kwa utaratibu wa Melkizedeki. Bwana yu mkono wako wa kuume; atawaponda wafalme siku ya hasira yake. Atahukumu kati ya mataifa, atajaza mahali maiti; ataziponda vichwa vingi juu ya nchi. Katika njia atakunywa maji mtoni; kwa hiyo atakiinua kichwa chake. Haleluya.
ZABURI 110
Nitakushukuru Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko. Matendo ya Bwana ni makuu; na shauri zake zote huchunguzwa, heshima na fahari ni kazi yake, na haki yake yakaa milele. Amekumbusha maajabu yake. Bwana ni mwenye rehema na mwenye huruma, anawapa wachao chakula; hukumbuka agano lake hata milele. Amewajulisha watu wake nguvu za matendo yake, awape urithi wa mataifa. Kazi za mikono yake ni kweli na hukumu. Maagizo yake yote ni amini, yamedumu milele na milele, yametendwa kwa kweli na unyofu. Ametuma ukombozi kwa watu wake, ameamuru agano lake hata milele. Jina lake ni takatifu na la kuogofya. Chanzo cha hekima ni kumcha Bwana, na ufahamu mwema ni kwa kila atendaye hayo, na sifaji yake yakaa milele. Haleluya.
ZABURI 111
Heri mtu amchaye Bwana, apendezwaye sana na amri zake. Uzao wake utakuwa hodari duniani. Kizazi cha wanyofu kitabarekiwa. Utajiri na mali zimo ndani ya nyumba yake, na haki yake yakaa milele. Nuru yawazukia wanyofu gizani. Bwana ni mwenye rehema na mwenye huruma na mwenye haki. Heri mtu anayefadhili na kukopesha, na atatengeneza mambo yake kwa haki, kwa maana hatatikisika milele. Kumbukumbu ya mwenye haki itakaa milele, wala hataogopa habari mbaya. Moyo wake u thabiti humtumaini Bwana. Moyo wake umethibitika hautatikisika hata atakapowaona adui zake. Amewagawia maskini. Haki yake yakaa milele. Pembe yake itakuzwa kwa heshima. Mwovu ataona na kuchukia, atasaga meno yake na kuyeyuka, tamaa ya mwovu itapotea. Haleluya.
ZABURI 112
Msifuni Bwana, enyi watumishi wa Bwana, lisifuni jina la Bwana. Jina la Bwana na libarikiwe, tangu sasa na hata milele. Tangu maawio ya jua hata machweo yake, jina la Bwana lisifiwe. Bwana yu juu ya mataifa yote, na utukufu wake juu ya mbingu. Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu?! Akaaye juu, aainamishaye ili autazame mbinguni na duniani, huwainua maskini kutoka mavumbini, na kumtua mhitaji kutoka jaani, awaketishe pamoja na wakuu wa watu wake. Humweka mwanamke tasa akae nyumbani, awe mama wa wana, afurahi. Haleluya.
ZABURI 114
Nampenda Bwana kwa kuwa alisikiliza sauti ya dua yangu. Kwa kuwa amelielekeza sikio lake kwangu; kwa hiyo nitamwomba siku zangu zote. Maumivu ya mauti yalinizunguka, mashaka ya Kuzimu yakanipata. Naliipata taabu na huzuni, nikaliita jina la Bwana: Ee Bwana, iokoe nafsi yangu. Bwana ni mwingi wa neema na mwenye haki, na Mungu wetu ni mwenye huruma. Bwana huwalinda watoto/wanyonge; niliyejinyenyekeza akanikoa. Rudi, nafsi yangu, kwenye raha yako, kwa kuwa Bwana amekutendea mema, akaikomboa nafsi yangu na mauti, macho yangu na machozi, miguu yangu na kuanguka, nitakwenda mbele za Bwana katika nchi ya walio hai. Haleluya.
ZABURI 115
Nilisadiki, kwa hiyo nikasema; mimi nimekewa sana. Nikasema katika haraka yangu: Wanadamu wote ni waongo. Nimlippie nini Bwana kwa ukarimu wake wote alionitendea? Nitalitwaa kikombe cha wokovu, nami nitaliita jina la Bwana. Nitalipa nadhiri zangu kwa Bwana mbele ya watu wake wote.
Ya thamani machoni pa Bwana ni kufa kwa wacha Mungu wake. Ee Bwana, mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako. Umezizikata pingu zangu. Nitakutolea dhabihu ya shukrani, nami nitaliita jina la Bwana. Nitalipa kwa Bwana nadhiri zangu katika nyua za nyumba ya Bwana, mbele ya watu wake wote, katikati ya Yerusalemu. Haleluya.
(Injili ya Luka 9:10-17) Na mitume waliporudi, wakamwambia mambo yote waliyoyafanya. Akawatwaa akaondoka nao faraghani mpaka mji uitwao Bethsaida. Makutano walipopata habari, wakamfuata; naye akawakaribisha, akawaambia habari za ufalme wa Mungu, akawaponya wale waliokuwa na haja ya kuponywa. Hata jua lilipoanza kutua, wale Thenashara wakamwendea, wakamwambia: Uache mkutano waende katika vijiji na mashamba yaliyo kandokando, wakapumzike na kujipatia chakula; kwa maana hapa tu mahali pasipo na watu. Akawaambia: Wapeni ninyi chakula. Wakasema: Hatuna kitu zaidi ya mikate mitano na samaki wawili, isipokuwa sisi twende tukajinunulie chakula kwa ajili ya watu hawa wote. Na walikuwako wanaume kama elfu tano. Akawaambia wanafunzi wake: Wakalishe chini kwa vikundi, watu kama hamsini hamsini. Wakafanya hivyo, wakawakalisha wote. Akatwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akavibariki, akavimega, akawapa wanafunzi wawaweke mbele ya mkutano. Wakala wote wakashiba; wakakusanya vipande vilivyowazidi vikapu kumi na viwili vilivyojaa. (Na utukufu uwe kwa Mungu daima)
INJILI TAKATIFU KULINGANA NA MT. LUKA (SURA 9:10-17)
Wale mitume waliporudi, walimweleza yote waliyoyafanya. Yesu akawachukua, wakaenda peke yao mjini Bethsaida.
Lakini wale watu walipojua alikokwenda, walimfuata. Yesu akawakaribisha akawazungumzia juu ya Ufalme wa Mungu, akawaponya wale waliohitaji kuponywa.
Jua lilipokuwa linaanza kutua, wale kumi na wawili walimwendea wakamwambia, "Waage watu waende kwenye vijiji na mashamba ya karibu, wakajipatie chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tulipo ni nyikani."
Lakini Yesu akawaambia, "Wapeni ninyi chakula." Wakamjibu, "Hatuna chochote ila mikate mitano na samaki wawili. Labda twende wenyewe tukawanunulie chakula watu wote hawa!"
(Walikuwepo pale wanaume wapatao elfu tano.) Basi, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Waambieni watu waketi katika makundi ya watu hamsinihamsini."
Wanafunzi wakafanya walivyoambiwa, wakawaketisha wote.
Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu.
Wakala wote, wakashiba; wakakusanya makombo ya chakula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
Tenoo oasht emmok o piekhristos nem pekyot en aghathos nem pi epnevma ethowab je akee ak soati emmon nai nan
Tunakusujudu, Ee Kristo, pamoja na Baba yako Mwema na Roho Mtakatifu, kwa kuwa umekuja na umetuoakoa.
1. Wewe uliyeionja mauti katika mwili saa ya tisa kwa ajili yetu sisi wenye dhambi, uziue tamaa za mwili ndani yetu, Ee Kristo Mungu wetu, na utuokoe. Ombi langu likaribie mbele zako, Ee Bwana; kwa neno lako unipe ufahamu. Dua yangu ifike mbele za uso wako; kwa neno lako unihuishi.
Doxa Patri ke Eioa ke Agio Pnevmati
Utukufu kwa Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu.
2. Wewe uliyekabidhi roho mikononi mwa Baba uliponing’inia msalabani, saa ya tisa, na ukamwongoza Mwivi aliyesulubiwa pamoja nawe aingie Paradiso, usinipuuze, Ee U Mwema, wala usinikatae mimi niliye potea; bali utakatifuze nafsi yangu na uangaze ufahamu wangu, na uniruhusu kushiriki neema ya mafumbo yako yenye kuhuisha; ili ninapoonja wema wako, nikupe sifa bila uvuguvugu, nikiitamani fahari yako kuliko vyote, Ee Kristo Bwana wetu, na utuokoe.
Ke nin ke a ee ke ees toos e onas toan e oa noan ameen.
Sasa na milele na hata milele ya milele, Amina.
3. Wewe uliyezaliwa na Bikira kwa ajili yetu, na ukastahimili kusulubiwa, Ee U Mwema, na ukaiondoa mauti kwa mauti yako, na ukaudhihirisha ufufuo kwa ufufuo wako, Ee Mungu, usiwaache wale uliowaumba kwa mikono yako mwenyewe, bali uonyeshe, Ee U Mwema, upendo wako kwa wanadamu. Kubali kutoka kwa mama yako maombezi kwa ajili yetu. Uokoe, Ee Mwokozi, watu wanyenyekevu. Usituache hata mwisho, wala usituache milele. Usivunje agano lako, wala usituondolee rehema zako, kwa ajili ya Ibrahimu mpendwa wako, Isaka mtumishi wako, na Israeli mtakatifu wako.
Ke nin ke a ee ke ees toos e onas toan e oa noan ameen.
Sasa na milele na hata milele ya milele, Amina.
4. Mwivi alipoona Mkuu wa Uzima akining’inia msalabani, akasema: “Kama yule aliyesulubiwa pamoja nasi asingekuwa Mungu aliyefanyika mwili, jua lisingeuficha mwanga wake, wala dunia isingetetemeka kwa kutikisika. Lakini, Ee Mwenyezi uvumiliaye yote, nikumbuke, Ee Bwana, utakapoingia katika Ufalme wako.”
Doxa Patri ke Eioa ke Agio Pnevmati
Utukufu kwa Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu.
5. Wewe uliyeikubali ungamo la Mwivi msalabani, utupokee nasi kwako, Ee U Mwema; sisi tunaostahili hukumu ya mauti kwa sababu ya dhambi zetu. Sote tunakiri dhambi zetu pamoja naye, tukikiri Uungu wako, nasi tunalia pamoja naye tukisema, “Utuikumbuke, Ee Bwana, utakapoingia katika Ufalme wako.”
Ke nin ke a ee ke ees toos e onas toan e oa noan ameen.
Sasa na milele na hata milele ya milele, Amina.
6. Mama alipoona Mwana-Kondoo na Mchungaji, Mwokozi wa ulimwengu, akining’inia msalabani, akasema akilia, “Ulimwengu unafurahi kwa kupokea wokovu, bali moyo wangu unaungua ninapotazama kusulubiwa kwako unakostahimili kwa ajili ya wote, mwanangu na Mungu wangu.”
Kisha mwabudu asali:
Bwana, utusikie, utuhurumie, na utusamehe dhambi zetu. Amina.
(Bwana utuhurumie) mara 41
Ondoleo
Ee Mungu Baba, Baba wa Bwana wetu na Mungu wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo, ambaye kwa kuonekana Kwake ulituokoa na kutukomboa kutoka utumwa wa adui; tunakuomba kwa Jina Lake kuu lenye baraka: uzihamishe akili zetu kutoka kujishughulisha na mambo ya dunia na tamaa za mwili, hadi kumbukumbu ya hukumu Zako za mbinguni; ukamilishe kwetu upendo Wako kwa wanadamu, Ee U Mwema. Na maombi yetu kila wakati, na sala ya saa hii ya tisa, yakubaliwe mbele Zako. Utujalie tuenende kama iwapasavyo mwito tuliouitiwa; ili tutakapotoka katika mwili huu, tuheshimiwe pamoja na wanaosujudia, wanaostahili mateso ya Mwanao wa pekee Yesu Kristo Bwana wetu; na tupate rehema, na msamaha wa dhambi zetu, na wokovu pamoja na safu ya watakatifu waliokupendeza kwa kweli tangu milele hata milele.
Ee Mungu, uibatilize kutoka kwetu kila nguvu ya mpinzani na jeshi lake lote baya, kama vile Mwanao wa pekee alivyozikanyaga kwa nguvu ya msalaba Wake unaohuisha. Utupokee kwako, Ee Bwana wetu Yesu Kristo, kama Ulivyompokea yule mwivi wa kuume ulipokuwa umening’inia juu ya mti wa msalaba; na utuangazie kama Ulivyowaangazia waliokuwa katika giza la Kuzimu; na uturudishe sote katika Paradiso ya neema; kwa kuwa Wewe, Ee Bwana wetu, Ndiwe Uliye barikiwa; nawe unastahili pamoja na Baba Yako Mwema na Roho Mtakatifu, utukufu, heshima, enzi, mamlaka na ibada hata milele. Amina.
Litania isomwayo mwishoni mwa kila saa
Utuhurumie, Ee Mungu, kisha utuhurumie. Wewe uliye katika kila wakati na kila saa, mbinguni na duniani, unasujudiwa na kutukuzwa, Kristo Mungu wetu Mwema, mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema, mwingi wa huruma, awapendaye wenye haki na kuwaonea huruma wenye dhambi, ambaye wa kwanza wao ni mimi; asiye taka mauti ya mwenye dhambi, bali aangamieje, apate kugeuka na kuishi; anayewaita wote katika wokovu kwa ajili ya ahadi ya mema yanayotarajiwa.
Ee Bwana, yakubali kutoka kwetu katika saa hii na kila saa maombi yetu; yafanye maisha yetu kuwa mepesi; utuongoze kutenda amri Zako; utakase roho zetu; usafishe miili yetu; uinue mawazo yetu; usafishe nia zetu; uponye magonjwa yetu na usamehe dhambi zetu; na utuopoe na kila huzuni mbaya na maumivu ya moyo. Utuzingire kwa malaika Wako watakatifu, ili tukiwa katika kambi yao tuhifadhiwe na kuongozwa, tupate kufika katika umoja wa imani na katika ufahamu wa utukufu Wako usiogusika na usio na mipaka; kwa kuwa Umebarikiwa hata milele. Amina.
Ee Mungu, utufanye tuwe waastahili kusema kwa shukrani: Baba yetu uliye mbinguni