TSK

TSK · Luka 21:36

مراجع Treasury of Scripture Knowledge في Swahili NT.

العودة إلى المقطع

Kisha Yesu akasema, "Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.

Muwe waangalifu na kesheni, maana hamjui wakati huo utafika lini.

Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.

lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.

Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.

Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.

Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.

Muwe macho; kesheni! Maana adui yenu, Ibilisi, huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mawindo.

Yuda 1:24 TSK

Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta ninyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake,